Friday, April 11, 2008

NDANI YA KUTANNE


Ukitaka kuyafurahia mapenzi, fanya hivi!

Ukitaka kujisikia raha kwenye mashamsham ya godoro, lazima ujue mengi. Mapenzi ni matamu sana iwapo unakutana na mwenzio mwenye kujua mapenzi, nasema hivyo kwasababu kumekuwa na malalamiko ya wanawake na wanaume wakilalamika kutoyafurahia mapenzi ya wapenzi wao. Kwanini usiyafurahie mapenzi ya mwandani wako,hebu jiulize ana matatizo gani?.Hakupendi ila analazimisha?.Maana kuna mwanaume mwingine kama hakupendi bwana kukuridhisha huwa tabu sana, labda avute hisia kutoka kwa yule ampendae lakini hivi hivi utaambulia patupu.Mwingine ni mvivu au hajui namna ya kumpenda mtu?. Looh, usishangae ukasikia mwanamke akisema jamaa yake akiingia uwanjani humaliza mpira kabla ya dakika tisini, ni mcheza kiungo hatari ambaye hana pumzi, dakika mbili hoi amemaliza mechi ya kwanza.Ukimbembeleza arudi jimbani anaanza kutoa visingizio lukuki, anaweza kutoa sababu kwamba anawahi sehemu muhimu, au atapiga simu akijaribu kutengeneza sababu ya kukutoka.

Kama wewe ni mwanamke ama mwanaume, huyo uliyosema unakutana nae faragha hakikisha unampenda sana, sio unampenda ilimradi amekuambia anakupenda, unajua kuulazimisha moyo useme uwongo ni ulimbukeni wa mapenzi kwani hutamfanya mwenzio akayafurahia Vitumbua vya nyama au Soseji.


Sasa basi, nataka nikufahamishe jinsi ya kutaka kuyafurahia mapenzi, ukiwa na mwenzako chumbani kabla ya kuingia dimbani, hakikisha kwamba mmejindaa kwa mechi, na kila mtu awe na hamu na nia ya kufunga mabao ya nguvu. Kabla ya kuingia uwanjani, wewe kama ni mwanamke unaweza kuja na Choculate nzuri ya baridi. Unaweza kununua ya maziwa, ya machungwa, ya mananasi,nk.

Kabla ya kunyonyana ndimi, unanawa mikono yako inakuwa safi kabisa, ukisha hakikisha mikono misafi, unapaswa kummegea mwenzio kipande kidogo cha Choculate ambacho utamlisha huku ukitabasamu kwa raha zako.Weee! mwanamke ameumbwa na tabasamu dear. Sasa usimbanie mwenzio kumzawadia tabasamu laini kama ute wa yai na jepesi kama pamba. Wakati unamlisha mweleze maneno mazuri ya mapenzi, unaweza kutumia lungha ambayo ataielewa vizuri, kama anajua. Akiwa anajua kizungu, Mwambie huku ukimwagia tabasamu," I beg you to love me the way you loved no one else"

Kwa kiswahili, unaweza ukatumia maneno haya, "Nakupenda, naomba unipende ambavyo hujawahi kupenda daima maishani mwako"

Ukimaliza nadhani hata yeye atasema, "Nakupenda, na nakuahidi sitokusaliti"Ukimaliza kumlisha mpatie ile chuculate ili nae akumegee kipande kidogo na akulishe kwa kutumia njia uliyotumia wewe. Ukishamaliza, kupeana choculate, unaweza kuasha kuila ile choculate kwa kuimumunya taratibu kutumia ndimi zetu.

Vipi, unaonaje hapo? Sasa tulia huu ni mwanzo, nitakupa vitu vikali mshikaji wangu!!!!


No comments: