Friday, April 11, 2008

BEMBELEZEKA...

Siri chumbani

Huyu ni Manka, mmh jamani Manka anawachanganya akina kaka, wajomba na hata wazee, oshiii! Kwa kifupi hana kasoro, ukibahatika kumuona na kumchambua ungeweza kudhani ukikufuru kuwa pengine mama yake aliamua kumuumba mwanaye mwenyewe na kuhakikisha amekuwa mzuri lakini ukweli kazi hii kubwa ya uumbaji ilifanywa na Mwenyezi Mungu pekee, mtoto ana kisura kilaini kama cha mtoto mchanga, ngozi nyororoo...sijui ana kula nini, meno meupe yenye mwanya wa wastani, akicheka hakika utapenda, wasichana wenziye wanamtamani, wanataka awe na umbo kama lake, wanaume wanaotaka kuoa wanaweke wazuri waliomuona wanachukulia mfano wa Manka, hana maringo hiyo ndiyo sifa yake kuu, ana umbo la kuwateka watu wa kila rika.

Siku hiyo alibaki mwenyewe, nyumbani kwake maeneo ya Sinza kwa Remmy, alikuwa alifanya usafi na baadaye akaendea bafuni kuoga, alijisugua na alipomaliza aliingia chumbani na taulo laini akajifuta maji mwilini na kuanza kupakaa mafuta ya kuirutubisha ngozi yake, kila alipojiona kiooni alimsifu mwenyezi Mungu kwa kazi nzuri ya uumbaji.

Mbele ya Dressing table yake iliyojaa vipodozi vya dharama, alitoa manukato ya J- Lo na mafuta ya Max Clare na St Elizabeth Aden, alipomaliza akapakaa uso wake ‘poda’ kidogo kisha akavaa sketi fupi inchi 12 na kitopu kilichoacha wazi kitovu chake kilichoingia ndani nusu inchi, hali iliyomfanya avutie sana, juu ya kitovu alikuwa na matiti makubwa kiasi yenye kuleta yaliyojaa na kusimama kwa kujitegemea ingawa alivaa sidiria.

Simu ikaita, akatembea kivivu na kuiokota, hakujua ni nani, zilikuwa namba mpya kutoka nje ya nchi.

“Haloo! Manka...Habari za Tanzania!” Sauti ya upande wa pili ilisikika.

“Nzuri, shikamoo!” Manka alishaijua sauti ya mtu aliyepiga.

“Jamani, si nilikuambia sipendi shikamoo, ok, unaendeleaje?” Ilikuwa sauti ya mzee Alex Ganza, mfanyabiashara maarufu jiji la New York na Afrika mashariki, ni mtanzania aliyezaliwa Kilimanjaro na kununua uraia Marekani.

“Safi! Nimekumisi sana Anko!” Manka alipenda kuita Anko, ingawa siri halisi hakuwa Anko.

“Mi’zaidi, naomba uniite mpenzi...Manka hukumbuki nilikulea ili uwe mke wangu!”

“Najua na nakuheshimu kama baba yangu, umenilea na nilikuwa nataka upate mkwe siku za karibuni!” Manka alisema , lakini kauli hiyo ikamtibua Alex.

“Mkwe! Nooo! Usiolewe na mwanaume mwingine, nitakuoa mimi, nakupenda Manka, toka ukiwa na siku moja duniani nilikulea, nataka nile matunda yangu..”

“Sijui kama itawezekana, tayari ninaye mwanaume ninayempenda!”

“Mwanaume gani mzuri kuliko mimi, mwanaume gani tajiri kushinda mimi, mwanaume gani ambaye angeweza kukuokota jalalani na kukusomesha hadi leo una elimu ya juu na unasimamia mali zangu? Wewe ndiye mke wangu, Manka...nakupenda!”Alilalaimika kimapenzi, Manka akajikuta akimuonea huruma, lakini bado alikuwa ana ampendaye.

“Ok, nimekuelewa, njoo basi tuongee vizuri, nakupenda wewe pamoja na huyo mpenzi wangu anayeitwa Boy...” Kauli hiyo ilimrufahisha nusu na kumuudhi nusu, iliyomchukiza ni kwamba anampenda pia Boy.

“Sawa, nimeota ndoto ya ajabu, usiku wa kuamkia leo!” Akabadili mazungumzo mzee Alex Ganza.

“Ndoto gani?”

“Siri ya Chumbani!”

“Unamaanisha nini, sijakuelewa mpenzi!” Naye akaamua kumfurahisha kwa kumuita mpenzi.

“Nikija nitakueleza, mapumziko mema mpenzi wangu!mmwaaa!”

“Na wewe pia! Mmmwaaaa!” Alimaliza na kukata simu.

******

Alipokata simu, akatafuta jina la mpenzi wake anayetingisha mtima wake na kumpigia, huyo ndiye aliyetaka kumkabidhi mwili wake auendeshe anavyotaka.

“Boy, njoo basi unipeleke kiwanja, ninazo hela za kutumia mpenzi wangu, njooo! Nipo nyumbani peke yangu,” alilalamika kikike akizungusha jicho la mahaba, jicho ambalo akikukata lazima apagawe na kudhani anakutamani, mtoto huyu! Mmh!.

“Poa, upo wapi?”

“Njoo nyumbani, msaidizi wangu wa kazi za ndani hayupo, nakupenda sana na usichelewa!”

“Nakuja usijali!”

“Mwili mzima unachemka, naomba ujiandae, kuna zawadi nitakupatia kwanza, ndipo twende zetu viwanja..njoo naumia!”

“Heeh! Unaumia kitu gani sweet!”

“Nakusubiri, usichelewa damu inachemka, natamani joto la karibu ...” kumbe Boy hakuwa mbali alikuwa maeneo ya Sinza madukani, akashuka kwenye daladala na kuelekea mtaa wa pili alikokuwa akiishia Manka, jumba la kifahari lililojengwa na Alex Ganza, alipofika alifungua mlango na kuingia hadi sebuleni ambako alimkuta Manka amejilaza sofani akiwa mweupe pee! Loh! Macho yakamtoka si kidogo, ilikuwa ni maajabu ambayo hakuwahi kukutana nayo, mtoto alifumba macho sijui alihisi baridi ama vipi, alikuwa amemtega si kidogo.

Siri Chumbani- 2

Baada ya kutoka bafuni, Manka msichana mwenye sifa zaidi ya mrembo anapigiwa simu na Alex Ganza, anamtaarifu kuwa anataka kurejea nchini huku akimuomba Manka asimuite anko na badala yake amuite mchumba, Manka anakataa akidai tayari anayealiyemchagua na kwamba anampenda sana.Je, ni mwanaume gani anayemchanganya Manka, Alex atafanya nini? Kumbuka huu ni mwanzo wa chombezo hilo la kusisimua......

Neno hili likapita tena akilini mwa Alex, “Sijui kama itawezekana, tayari ninaye mwanaume ninayempenda! Pole sana Alex!” Akauma meno na kukunja ndita, kuliko kumkosa Manka ilikuwa afadhali kufa, alimdharamikia sana na kumlea mpaka alipofikia hapo anatamaniwa na mwanaume mwingine, siri kubwa ya Manka aliifahamu.

Sekunde kadhaa alizokaa kimya, akazinduka mithili ya mtu aliyetoka katika ndotoni ya kutisha na kusema jasho likimtoka.

“Mwanaume gani mzuri kuliko mimi, mwanaume gani tajiri kushinda mimi, mwanaume gani ambaye angeweza kukuokota jalalani na kukusomesha hadi leo una elimu ya juu na unasimamia mali zangu?

Wewe ndiye mke wangu, Manka...nakupenda!”Alilalamika kimapenzi, Manka akatulia akimsikiliza kwa makini, ingawa hakuwa na uhakika kama aliokotwa jalalani lakini mwanaume huyo ndiye aliyemlea kama mzazi wake, alimsomesha na kumkabidhi mali zake azisimamie, siku zote alimheshimu na asingependa kuolewa na mtu toka utotoni mwake alimuita Anko.

Roho ya huruma ikamuingia, akabaki njia panda kuendelea na mwanaume huyo ama kuendelea na kipenzi chake, moyo ukakataa na kudai kuwa, “Umemchagua John Mule, basi huyo ndiye unayetakiwa kuwa naye,” sauti kutoka moyoni iliendelea kumsihi.

“Manka...nisikilize basi mpenzi!” Sauti ya Alex ilisikika, lakini ya chini na ya kubembeleza.

“Mmh! Sawa nimekuelewa, njoo basi tuongee vizuri, nakupenda wewe pamoja na huyo mpenzi wangu anayeitwa John...” Kauli hiyo ilimrufahisha Alex nusu na kumuudhi nusu, iliyomchukiza ni kwamba anampenda pia John.

“Sawa, nimeota ndoto ya ajabu, usiku wa kuamkia leo!” Akabadili mazungumzo mzee Alex Ganza.

“Ndoto gani?”

“Siri ya Chumbani!”

“Unamaanisha nini, sijakuelewa mpenzi!” Naye akaamua kumfurahisha kwa kumuita mpenzi, na kweli Alex alifurahi sana, pesa kwake zilikuwa hazina maana bila Manka.

“Nikija nitakueleza, mapumziko mema mpenzi wangu!mmwaaa!”

“Na wewe pia! Mmmwaaaa!” Alimaliza na kukata simu, Manka akamuwaza tena muhibu wake, kila alipomuwaza alikosa hamu ya kula na kuhisi kama vile mgonjwa.

******

Alipokata simu, akatafuta jina la mpenzi wake anayetingisha mtima wake na kumpigia, huyo ndiye aliyetaka kumkabidhi mwili wake auendeshe anavyotaka, alitaka kula raha za dunia akiwa na John Mule.

“John, njoo basi unipeleke kiwanja sasa hivi, ninazo hela za kutumia mpenzi wangu, njooo! Nipo kitandani peke yangu,” alilalamika kikike akizungusha jicho la mahaba, jicho ambalo akikukata lazima apagawe na kudhani anakutamani, mtoto huyu! Mmh! Jamaniii anamvuto kila mahala.

“Poa, upo wapi?” Sauti nzito ya kiume na iliyopoa ilisikika, moyo wa Manka ukapasuka paaa’ hizia za huba zikamuingia mara moja.

“Njoo nyumbani, msaidizi wangu wa kazi za ndani hayupo, nakupenda sana usichelewa mpenzi!”

“Nakuja usijali!”

“Dakika ngapi?” Manka alihoji, ili ajiandae haraka na kuonekana mpya, si unajua tena wawili wawapo faragha lazima wajiandae fresh?.

“Robo saa,” alimjibu akihisi moyo ukimdunda.

“Mwili mzima unachemka, naomba usichelewe kuna zawadi nitaka nikupatie kabla hatujatoka OUT..njoo dear naumia!”

“Heeh! Unaumia kitu gani sweet!”

“Nakusubiri, usichelewa damu inachemka, natamani joto la karibu ...” kumbe John hakuwa mbali alikuwa maeneo ya Sinza madukani, akashuka kwenye daladala na kuchukua teksi mara zote Manka alimuonya kutopanda daladala, hiyo akajua ni sooo kuingia jumba la Manka na kumi na moja zake.

Jumba hilo juu lilikuwa na mnara uliandikwa Alex Ganza, walinzi walikuwepo wa kutosha kabisa, alipofika na kwakuwa alifahamika na walinzi, alifungua mlango pua zake zikakubwa na gharika la manukato yaliyopoa na yenye kuvutia, akatembea taratibu sebuleni ambako alimkuta Manka amejilaza sofani akiwa mweupe pee! Loh! Macho yakamtoka si kidogo, ilikuwa ni maajabu ambayo hakuwahi kukutana nayo, mtoto alifumba macho sijui alihisi baridi ama vipi, alikuwa amemtega si kidogo.

Alipofika John alipiga magoti na kuisogeza kichwa chake katika kitovu cha Manka, akatasua midomo iliyojaa mate ya huba na kumbusu mara mbili akapata taratibu huku akimwita Manka jina lake, kumbuka sauti hiyo iliendelea kuwa nzito la kimapenzi.

“Mankaa...unaniga mamaaaa...sweeetii naomba nikufunike...” Ndani ya sebule hiyo ya kifahari kulikuwa na kiyoyozi cha kotosha kabisa, wote wakawa wanapigwa na ubaridi fulani.

Taratibu mkono usio na adabu wenye kutekenya ulipita ukitalii taratibu na kufikia hatua ya kumfanya Manka afumbue macho ya ya kurembua.

“Hey sweet umekuja mpenzi wangu, nashukuru karibu,” Manka aliinuka na kumkaribisha John aketi sofani, baadaye akakibamba kila mmoja alimbamba mwenye kiuno wakaingia chumbani ambako Manka hakutaka kitu kingine zaidi ya zawadi aliyomwandalia mpenzi wake kwa muda huo.

“Mbona unazima simu mpenzi...” Manka alimuuliza, akijitupa kitandani, naye John akafuatia.

“Si unajua mambo haya hayahitaji usumbufu, hivi simu ikiita nikawa katikati ya bustani napalilia mboga mboga, si itanikata ‘stimu’,”

“Poa, si unaiacha iite mpaka ikatike, naona wivu!” Alisema akipitisha mikono yake kifuani mwa John aliyeanza kuongea kwa sauti nzito huku Manka sauti yake ikiwa nyororo zaidi, kila mtu alikuwa na shauku ya palilia bustani na kuhakikisha bustani yao inakuwa bora, kwani walihitaji kupanda mmea, wenye rutuba na utakao mfariji kila mmoja aibuke na faraja moyoni, mmh! Sijui mwiye nahadhia.

“John...taratibu, mashuka meupe...” ilikuwa sauti ya Manka akijipindua upande wa kaskazini baada ya kuona mwenyeye ana kasi katika kucheza mduara.

“Mashuka meupe.. taulo inachafuka wakati mtu ametoka bafuni kuoga, acha yachafuke baby...”

“Nina zawadi nyingine...” Manka alisema kwa sauti ya kitetemeshi mapigo ya moyo yakienda kasi.

“Ipi!”

“Subiri, ulishawahi kukutana na mwanamke mwenye mapengo ya mbele...” Alisema Manka.

“Hapana!” Manka akainuka kwenda bafuni alipotoka alikuwa amefanya usafi, mapengo yake ya mbele katika meno manne yalionekana safi na yakupendeza.

Hakujua, kumbe meno ya dhahabu ya Manka yalikuwa si urembo bali hakuwa na meno, akasogeza midomo yake na kugusanisha na midomo ya John. Hapo alikuwa mambo mengine kabisa, usijaribu! John alipagawa na kuchanganyikiwa, kwani ulimi wake haukupata tabu katika kutalii na kubadilishana mate.

Baadaye wakati John akiwa hoi taabani, Manka akatoa choculate kwenye jokofu na kummegea John kisha kumlisha na John akammegea Manka kipande kidogo, wakaanza kumumunya taratibu hali iliyowachanganya na kuwafanya warukwe na akili. Kuanzia siku hiyo, wote walichanganywa katika penzi na kutamani kukutana kila mara.

“Tulale kwanza kisha baadaye twende Club Billicanas” Alishauri Manka lakini mambo aliyopewa ya muda mfupi na Manka yalimchanganya. John hakutaka kulala alitaka kuendelea kurina asali.

********

Siku alipozaliwa Manka, ndipo mama yake kwa bahati mbaya alifariki na kumuacha Manka aliyelelewa hospitalini, na baadaye akachukuliwa na baba yake hadi nyumbani akaletewa wasichana watatu wa kumlea, hiyo yote ilifanywa na Alex Ganza, baba yake Manka.

Siku zote, Alex alihakikisha mwanaye wa pekee hajui siri hiyo, wasichana hao wa kazi aliwafahamisha kuwa wasije kuifichua siri hiyo, akiwa chekechea mzee Alex alionekana kumtamani sana mwanaye aliyefanana na marehemu mchumba wake, Angela. Msichana Angela alikuwa ni mchanganyiko wa mzungu na mwafika, kila kitu Alex alikifanya siri. Manka alipofikisha umri wa miaka saba alijaribu kumuuliza Alex kama mama yake alikuwa wapi na yeye ni nani wake, kwa hisia Alex akamweleza Manka kuwa siku moja usiku wa manane akiwa anatembea alisikika mtoto akilia jalalani, aliposimama aliweza kugundua mahala alipo, alichokifanya ni kutembea hadi jalalani na kumuokota mtoto aliyekuwa amebabuka mwili kwa joto na kuhifadhiwa kwenye mfuko wa plastiki.

“Mmh! Mtoto huyo alikuwa nani?”

“Huwezi kuamini, wewe ndiye niliyekuakota na kwa vile sikuwa na mke wala mtoto nilihakikisha nakulea vizuri na baadaye uwe mke wangu!” Alisema Alex kwa hisia kali, alimdanganya mwanaye mpendwa. Alikuwa mzuri sana na kumfanya aingiwe na hisia za ajabu.

Itaendelea