Friday, April 11, 2008

Ndani ya kuta nne, hakuna shahidi...


Mapenzi ni sawa na mgonjwa, lazima apewe Dozii ya uhakika...Sasa wewe unasubiri nini? Mpe dozi mwenzako usimchoshe....atakukimbia...shauri yako....

Nimatumaini yangu wapenzi wasomaji ya mahaba ni wazima wa afya na mnaendelea vema na shughuli zenu za kila siku.Mi nimzima na namshukuru Mungu kwa kunijaali afya njema. Leo napenda kugusia umuhimu wa Romance.

Kabla ya yote unaweza kujiuliza nini maana ya Romance, kwa kulitamka neno Romance nirahisi sana lakini kulijibu ni vigumu, jaribu utaona kama unaweza kusema nini maana ya Romance. Ni kitu ambacho unaweza kufanya na mpenzi wako, wakati mkiwa faragha, unaweza kutumia muda mwingi mkitomasana ama kupeana vitu ambavyo vitawafanya kuwa karibu zaidi. Romance ni muhumu sana katika maisha ya mapenzi, bila romance maisha yako ya mapenzi hayataweza kudumu. Pia romance ni uthibitisho wa kweli katika mapenzi yenu. Inaonyesha mapenzi yako ya kweli na inakusaidia kuwa mpenzi mzuri kwa mwandani wako.

Mara nyingi siku zinavyokwenda watu wengi husahau kuwapa wapenzi wao Romance nzuri ambayo itawavuta karibu na kuwafanya wajisikie furaha kila wanapokuwa mbali na wapenzi wao, hivyo Romance wakati mwingine huvuta hisia za mapenzi hata kama mpo mbali kimwili lakini kifikikra na hisia zinaweza kuwavuta karibu mkakumbukana kwa yale mliyokutendeana siku moja mlipokuwa faragha.

Kuna njia ambazo unaweza kuzifanya kuweka mshumaa wa romance ambao utakuwa ukiwaka moyoni mwako maishani. Ukakufanya usijute kuwa na mwandani wako, utajiona chaguo lako lilikuwa bora zaidi.

Nini cha kufanya kwa mpenzi wako Kila siku?

1. Mwambie mpenzi wako kiasi gani unavyompenda, sio kukaa kimya, atajuaje kwamba unampenda.

2. Mwambie 'Nakupenda sana' hata mara saba kwa siku, atajisikia furaha moyoni na hata kama alikuwa na wasiwasi na wewe sasa utakuwa wakati wakuamini kiasi gani unavyompenda.

3. Tumia angalau muda mchache wa kuwa nae sehemu tulivu mkipota vinywaji baridi na chakula, pia mtalazimika katika sehemu hiyo tulivu mjadili mipango yenu ya maisha, unaweza kutumia hata saa moja kwa mazungumzo au hata zaidi ya saa moja, sio unaenda dakika mbili unaondoka. Atakuona unakuja kumsanifu au unamuwahi mwingine, kama una kazi ya muhimu mweleze taratibu kwamba una kazi, hatabisha kama ni muungwana. Atakusikiliza na mtapanga labda kukutana kesho utakapokuwa na nafasi, tena hakikisha unatafuta muda wa kuwa na mpenzio.

4. Mfanyie Surprise au kitu ambacho hakikutarajia akilini mwake. Unaweza kumletea zawadi nzuri sana, labda simu ya mkononi, nguo ya ndani, au kitu chochote ambacho unajua hakikuwa akilini mwake.

5. Kama mnaishi pamoja, mnapoamka asubuhi unatakiwa umkumbatie mpenzio, mkeo au mumeo. Unaweza kumsifu kwa kazi ya jana ambayo kwa kiasi kikubwa uliifurahia, usimbanie kuhusu suala la kumsifia. Mpe moyo kwamba anayaweza mashamsham ya gadoro, au vipi? mpenzi msomaji.

Nini cha kumfanyia mpenzio kila wiki?

1.Umanatakiwa kupeana miadi ya kwenda mahala tulivu kabisa, mkibadilisha na mawazo. Sio kila siku kuwa chumbani, unachotakiwa ni kubadilisha mazingira. Wakati unapokuwa mnaelekea labda sehemu ya kubadilishana mawazo, usipende kutembea eti, mume nyuma mke mbele, kwani unamwogopa nani? Waonyeshe wale wanaojua kuchukua vya watu kwamba mmejenga ukuta imara wa penzi lenu. Watashindwa kutupa ndoana za kukuteka wewe ama mpenzio, Shikaneni mikono tena mkionyeshana kiasi gani mnapendana.

2. Mfanyia kitu ambacho wote mnaweza kukifurahia kwa kikifanya kwa pamoja.

3 Kama ni mwanamke unaweza kumpikia chakula kizuri ambacho anapendelae kukila, hakikisha chakula hicho kuanzia mapishi hadi kukiandaa mezani ni kazi yako. Sio Umpikie halafu umwambie 'hausigeli' akamwandalie, haipendezi kabisa na hata jisikia kula chakula chako. Siajabu hata siku hiyo ya wikiendi unaweza kumlisha chakula hadi akashiba, sio kazi kumlisha mpenzio, unajua mwanaume ukimnyenyekea hukisikia ni bora na huongeza mapenzi zaidi.Atakudhamini kuliko chochote, atapenda kukuona mara kwa mara.

Mimi binafsi na mlisha mepnzi wangu, kwani nampenda sana. Ninapomlisha chakula akishiba nae hunilisha kwa furaha. Ninapomtamkia nimeshiba basi hunitolea tabasamu nono lililoshiba midomoni mwake.

4. Mpe mpenzio zawadi ya kumshangaza, ambayo unahisi ataipenda na kuifurahia.

5.Fikiria kitu ambacho utamfanyia wiki nyingine, hasa mapenzi. Usifanye mapenzi kila siku na pia hakikisha unabuni njia nyingine mpya ambazo atazipenda na kuzifurahia.

Nini cha kufanya kila mwezi?

1.Unaweza kutoka na mpenzio mkaenda kufanya Shopping na ukamnunulia zawadi nzuri, kama nguo, viatu, nk.

2.Mnaweza kutizama mkanda wa mahaba, angalau mara mbili kwa mwezi. Hakikisha wakati wa kuangalia mkanda, unamwonyesha staili nzuri uzipendazo. Usione aibu kumwambia unaipenda staili moja kati ya mbili, tatu ulizochagua.

3. Unashauriwa kwenda na mpenzio kucheki afya zenu kila baada ya miezi miwili, hii itasaidia kama kuna magonjwa basi yapatiwe tiba, sio unasema unampenda mwenzio lakini mumshauri kupima afya zenu.

4. Muulize kitu ngani labda ambacho umemfanyia bila kujua kama umemuudhi, kwani wakati mwingin e unaweza kumuudhi mwenzio bila kujua na kukaa kimya kwako kutamfanya aendelee kuumia.

Hebu ukiwa na mpenzi wako jaribu kubadilika bwana, sio kukaa kama gogo au ukimaliza mtanange unakimbilia kufuli, la nini, halina kazi tena ukiwa na mwandani wako...hebu mpe faraja nzito.....aliwazike hakuna kubaniana...

3 comments:

Ema said...

Hi nimeipenda bro!
So interesting

Unknown said...

Interesting, shida yaja kwa mwanaume anaedhani anajua kila kitu kitandani na ukijaribu kumwelekeza jinsi ya kukufurahisha ni shida. Halafu mgumu kweli kweli, alivyozoea yeye ndio hivyo hivyo hakuna kubadilika, hadi inakera. wanawake wengine tupo tayari kujaribu new styles ili kufurahiana na wezi wetu ila mwanaume hataki kujaribu style tofauti. Kazi yake ni kukucriticize tu kila wakati. Mwisho wake hapo kitakua nini?

🌎 said...

Sikuwahi kuamini kitu kama hiki kingeweza kunitokea hadi ndoa yangu ilipokaribia kuisha kabisa.

Mume wangu alibadilika ghafla. Mwanaume ambaye hapo awali alinipenda na kunijali akawa baridi, asiyejali, na mwenye hasira bila sababu. Aliacha kuonyesha nia katika ndoa yetu, akaniepuka kabisa, na hatimaye akaniomba talaka. Nilivunjika moyo kwa sababu nilimpenda mume wangu kwa moyo wangu wote.
Mambo yalizidi kuwa mabaya aliponizuia kila mahali — WhatsApp, Facebook, Instagram — kana kwamba sijawahi kuwepo. Nililia kila usiku nikijiuliza nilifanya nini kibaya.
Siku moja, rafiki wa karibu alinitembelea na kunitambulisha kwa mtu wa kiroho anayeitwa Dkt. Dawn. Kwa kweli, mwanzoni nilikuwa na shaka, lakini niliamua kumweleza kila kitu kwa sababu sikuwa na chochote cha kupoteza.

Dkt. Dawn alinisomea mambo ya kiroho, na nilishtuka. Alifichua siri kuhusu ndoa yangu na maisha yangu binafsi ambayo hakuna mtu aliyejua. Kila kitu alichosema kilikuwa sahihi 100%. Kisha akafichua kwamba mwanamke mwingine alikuwa amemloga mume wangu. Mwanamke huyu alikuwa akimtembelea mara nyingi, na kwa upumbavu niliamini ilikuwa kuhusu kazi tu.
Dkt. Dawn alinisaidia kuvunja uchawi na akafanya ibada yenye nguvu ya kurejesha upendo kwa ndoa yangu.
Kwa mshangao wangu mkubwa, muda mfupi tu baadaye, mume wangu alinifungulia kizuizi mwenyewe na kuanza kunipigia simu na kunitumia ujumbe mwingi, akiniomba nimsamehe na nirudi nyumbani. Mwanzoni nilimpuuza kwa sababu ya maumivu aliyonisababishia, lakini hatimaye alirudi nyumbani akiwa na zawadi na machozi machoni mwake akiomba nafasi nyingine.
Leo, ndoa yetu ni imara zaidi, yenye furaha zaidi, na yenye amani zaidi kuliko hapo awali. Mapenzi kati yetu yanahisi upya kabisa.
Kana kwamba hiyo haitoshi, Dkt. Dawn baadaye alinisaidia na ibada ya ujauzito kwa sababu tulikuwa tumejitahidi kwa miaka mingi kupata watoto. Ndani ya wiki 8, nilipata mimba kiasili, na leo tumebarikiwa na wavulana wawili wazuri wenye afya njema.
Nitaendelea kushukuru milele.
Ukihitaji: Uchawi wa mapenzi wa kuungana tena na mpenzi wako wa zamani
. Usaidizi wa kurejesha ndoa
. Tamaduni za ujauzito za kupata mimba
. Usaidizi wa kiroho kwa kesi za mahakamani au kupona urithi
. Mwongozo na ulinzi wa kiroho
Ninapendekeza sana Dkt. Dawn. Ushuhuda wangu ni wa kweli, na furaha yangu leo ni uthibitisho. WhatsApp yake: +2349046229159
dawnacuna314@gmail.com